DHANA YA UHURU NA HARAKATI ZA KUDAI UHURU
Uhuru ni hali ya mtu au nchi kuamua na kufanya
mambo yake bila kuingiliwa na mtu au taifa lolote iwe kiuchumi, kisiasa,
kijamii au kiutamaduni.
Katika
muktadha huu;-
Uhuru
ni hali ya nchi kujikomboa kutoka kwenye ukoloni wa mataifa ya kibepari.
Harakati za
kudai uhuru
Ø Harakati za kudai uhuru wa Tanganyika
na Zanzibar ni mchakato au juhudi za watu wa nchi
hizo kutafuta uhuru kutoka kwa serikali za kikoloni.
Ø AU ni ni hatua
zilizochukuliwa na wananchi wa Tanganyika na Zanzibar ili kufanikisha kupata
uhuru wao kutoka kwenye utawala wa kikoloni.
v Tanganyika
ilitawaliwa na:-
i.
Wakoloni
wa kijerumani kuanzia mwaka 1885 hadi 1918.
ii.
Wakoloni
wa Uingereza kuanzia mwaka 1919 hadi ilipopata uhuru mnamo mwaka 1961.
v Zanzibar
ilitawaliwa na:-
i.
Utawala wa kisultani kutoka oman kuanzia
mwaka 1840 hadi 1890,
ii. Utawala wa Waingereza kuanzia mwaka 1890 hadi
1963.
MISINGI YA KUDAI UHURU WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR
Ø Watanzania
walianzisha harakati za kudai uhuru baada ya kuanzishwa kwa serikali za
kikoloni.
Ø Sababu zilizosababisha watanzania
kudai uhuru wao ni kama ifuatavyo:
a)
Unyonyaji wa mali na rasilimali:
Mfumo
wa kikoloni ulikuwa wa kiunyanyasaji na kinyonyaji. Watanzania walinyonywa
katika nchi yao.
Ø Mathalani
walifanya kazi katika maeneo mbalimbali kama vile mashambani , migodini n.k
bila kupata ujira unaostahili.
Ø Vile
vile waliamuliwa kulima mazao yaliyoletwa na wakoloni kwa ajiri ya viwanda
vyao.
Ø Hali
hii ilijenga msingi mmojawapo katika harakati za kudai uhuru wa Tanganyika na
Zanzibar
b)
Sera za kibaguzi:
Sera
mbalimbali za kibaguzi zilianzishwa kupitia huduma za jamii, kwa mfano wananchi
walibaguliwa katika kupata huduma za jamii kama vile afya, elimu na makazi.
Ø Wazungu,
Waarabu na Waasia walipewa huduma bora wakati Waafrika wakipewa huduma duni au
kutopewa kabisa.
c)
Ukandamizwaji wa
waafrika:
Wakoloni
walipofika walianza kupora ardhi nzuri ya uzalishaji mali kutoka kwa wenyeji.
Ø Hivyo
iliwalazimu wenyeji hao kufanya kazi katika mashamba ya kikoloni ili waishi, na
walilipwa ujira kidogo au amna kabisa.
Ø
Pia
wananchi walitozwa kodi kwa nguvu. Lakini pia walilazimishwa kujenga
miundombinu mbalimbali mfano reli kwa nguvu
d)
Kudhihakiwa kwa mila na desturi za watanzania:
Wakoloni kupitia wamisionari walipiga marufuku mila za
kiafrika. Kwa mfano majina pamoja
na dini za kiafrika zilionekana ni za kishenzi,
Ø
Pia baadhi ya vyakula, nguo, lugha na
sanaa vilipigwa marufuku.
e)
Kuongozwa na wakoloni:
Wakoloni
walitaka kutawala Tanganyika na Zanzibar kwa muda mrefu, hivyo mifumo ya
kiutawala haikutoa nafasi kwa waafrika kuendelea na utamaduni wao wa kuongozwa
na viongozi wao wa jadi. Hali hii iliondoa uhuru wa watanzania.
Ø Hata
pale viongozi wa jadi walipokuwa wakitawala kupitia mfumo wa uwakala, uamuzi
wotw ulitolewa na wakoloni kupitia gavana, wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya.
Ø Hali
hii iliwakasirisha Watanganyika na kuamua kuanzisha harakati za kudai uhuru.
MBINU ZILIZOTUMIKA KUDAI UHURU WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR
Ø Harakati
za kudai uhuru waTanganyika na Zanzibar zilitumia mbinu mbalimbali, ikiwa ni
pamoja na kuanzisha jumuiya, vyama na taasisi za kijamii za waafrika.
Ø Malengo
ya kuanzishwa kwa jumuiya, vyama na taasisi hizo yalikuwa ni kutetea na kudai
haki za wafanyakazi, wakulima na wafanyabiashara.
Ø Kadri
muda ubavyoendelea, jumuiya vyama na taasisi hizo zilijihusisha na siasa na
kuchangia sana katika harakati za kudai uhuru wa Tanganyika na Zanzibar
A: VYAMA
VYA USHIRIKA NA WAKULIMA
Chama cha ushirika
ni muungano wa watu waliokubaliana kuendesha shughuli zao za kiuchumi kwa
pamoja ili kuinua hali zao za maisha.
Ø Shughuli
hizi ni kama vile kutafuta mahitaji yao ya chakula, elimu, uuzaji wa mazao yao
na shughuli nyingine za uchumi zinazoweza kuendeshwa kwapamoja.
Ø Vyama vya wakulima
vilianzishwa na wakulima wenyewe katika maeneo ambapo mazao ya kibiashara
yalilimwa.
Malengo
ya vyama vya wakulima ni ;-
i.
Kudai
bei nzuri ya mazao yao ,
ii.
Kupata masoko ya uhakika,
iii.
Kudai
pembejeo na zana za kilimo,
iv.
Kupinga unyonyaji na kutozwa kodi kubwa ya
mazao yao.
Mifano ya vyama vya
wakulima ni Bukoba Buhaya Union(1924), Kilimanjaro native Planters Association
(1925), Sukuma union (1930), Pare union (1949)
Ø Kwa
upande wa Zanzibar, kulikuwa na jumuiya mbalimbali zilizoundwa na makundi ya
wakulima kwa malengo kama ya wenzao Tanganyika.
Ø Vyama
hivi vilitoa watu mbalimbali ambao walikuja kuwa viongozi wa kisiasa, kama Paul
Bomani na Clement George Kahama.
Ø Vilevile
vyama hivi vilipinga uamuzi wa serikali ya kikoloni ambao ulikuwa
unawakandamiza watanganyika na wazanzibar.
Ø Vyama
hivi pia vilitoa pesa kwa TANU, kuunganisha na kuhamasisha watu katika harakati
za kupigania uhuru wa Tanganyika.
B: VYAMA
VYA WAFANYAKAZI
Ø Waafrika
waliokuwa wameajiriwa katika viwanda, mashamba, bandari na sehemu nyingine
walianzisha vyama vyao vya wafanyakazi kwa lengo la kulinda na kutetea masilahi
yao ya kikazi.
Ø Mfano
wa vyama vya wafanyakazi ni;-
·
Tanganyika Territory Civil Servants’
Association(TTCSA), kilichoanzishwa na Martin Kayamba mwaka 1922 huko Tanga,
ambapo mwaka 1924 kilifungua tawi lake mjini Dar es Salaam.
·
Dock Worker’s Union(1937)
·
Railway African Civil Service Union(1920)
·
Tanganyika Federation of Labour (1955)
chini ya uongozi wa Rashid Mfaume Kawawa.
Ø Kwa
upande wa Zanzibar kulikuwa na;-
·
Jumuiya ya mabaharia kwa ajiri ya
kupigania haki za wafanyakazi katika vyombo vya baharini. Jumuiya hii iliundwa
na Sheikh Abeid Amani Karume Mwaka 1939.
·
Federation of Zanzibar and Pemba Trade
Unions (ZPFL) 1956.
Ø Pamoja
na juhudi zao za kutetea masilahi ya wafanyakazi, waliendelea kujadili masuala
ya kisiasa na hatimaye walijihusisha na harakati za kudai uhuru
C: VYAMA
VYA WAFANYABIASHARA
Vyama
vya wafanyabiashara wa Kiafrika vilianzishwa nchini Tanganyika ili kuyalinda na
kuyatetea masilahi ya wafanyabiashara wa kiafrika dhidi ya wafanyabiashara wa
kigeni
Ø Baadhi
ya madai yao ilikuwa ni kupinga unyanyasaji katika masoko, kupinga kutozwa kodi
kubwa n.k
Ø
Mfano
wa vyama hivi ni African Commercial Association kilichoanzishwa mwaka 1934
chini ya Erica Fiah.
Ø
Kwa
upande wa Zanzibar, kulikuwa na Jumuiya ya Wahindi iliyoundwa mwaka 1910.
Ø
Vyama
vya kijamii viliendelea kukua mwaka hadi mwaka nchini Tanganyika na Zanzibar.
Mfano wa vyama hivi ni Tanganyika African Association (TAA) kilichoanzishwa Dar
es salaam mwaka 1929. Chama cha TAA kiliundwa na watumishi wa serikali na
baadaye kikazaa chama cha siasa kiitwacho TANU.
Ø
Zanzibar
kulikuwa na African Association na Shirazi Association. Jumuiya hizi ziliungana
na kuunda Chama cha Ukombozi cha Afro-Shirazi Party (ASP) ambacho pia ndicho
kiliungana na TANU kuunda chama cha mapinduzi (CCM) mwaka 1977
Ø
Pamoja
na kutetea haki na masilahi ya wafanyabiashara, vyama hivi vilikuja kushiriki
katika harakati za kudai uhuru, ikiwa ni pamoja na baadhi yao kubadilika na
kuwa vyama vya siasa
D: VIKUNDI NA VYAMA VYA KIDINI
Dini
za kikristo na kiislamu zilitumika kama vyombo vya kuwaunganisha watu na
kuendeleza harakati za kudai uhuru Tanganyika na Zanzibar.
Miongoni mwa vikundi na vyama vya kidini vilivoanzishwa
nchini Tanganyika ni;-
·
Al-
Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (1933),
·
The Watch Tower Church,
·
The African National Church
·
The Church of God
Ø Vikundi
hivi vilitoa viongozi shupavu kama Ally Sykes, Bibi Titi Mohamed, Tewa Said
Tewa na wazalendo wengine ambao walishirikiana na mwalimu JK Nyerere katika
mapambano ya kudai uhuru wa Tanganyika
E: VILABU VYA MPIRA WA MIGUU
Vilabu
vya mpira wa miguu vya Waafrika vilianzishwa na kusaidia kuimarisha umoja na
mshikamano miongoni mwa Waafrika sambamba na kueneza fikra za ukombozi dhidi ya
madhila ya wakoloni.
·
Zanzibar mwaka 1931 ilianzishwa klabu ya mpira wa miguu ,The African sport club
ambayo kiongozi wake alikuwa sheikh Abeid Amani Karume .
·
Kwa upande wa Tanganyika, mwaka 1935
ilianzishwa klabu ya waafrika yenye jina la Young African Sport Club
Ø Vilabu
hivi vilihamashisha waafrika kujiunga na vyama pamoja na jumuiya kama vile TAA.
Pia vilitoa michango mkubwa wa kuchangisha fedha kwa wanachama wao pamoja na
kuwahamasisha kujiunga na vyama vya TANU na ASP
F: VYOMBO
VYA HABARI
Kuanzishwa
kwa vyombo vya habari Tanganyika na Zanzibar kuliongeza na kuimarisha harakati
za waafrika katika kupigania uhuru wao.
Ø Kwa
upande wa Tanganyika, mfano wa vyombo hivyo ni;-
·
Gazeti la kwetu, lililoanzishwa na jumuia
ya African Association (AA) mwaka 1937.
·
Sauti ya TANU, ambalo lilihaririwa na Mwalimu
J.K Nyerere mwaka 1957.
Ø Kwa
upande wa Zanzibar kulikuwa na, kwa mfano,
·
Gazeti
la Sauti ya Zanzibar (1949)
·
Gazeti
la samachar lililoandikwa na Bwana Mtoro bin Abu Rehan
·
Magazeti
mengine ni Afrika kwetu, mwongonzo, jasho letu, mkombozi, mwiba, sauti ya
afro-shirazi, sauti ya jogoo na umma
Ø Vyombo
vya habari vya Waafrika vililenga kuamsha ari ya uzalendo kwa Watanganyika na Wazanzibar
ili kuwaunganisha katika kudai uhuru wao.
Ø Aidha
vilitumika kupaza sauti dhidi ya maovu yaliyokuwa yakifanywa na serikali ya
kikoloni
G: VIKUNDI NA VYAMA VYA SANAA
Wakati
wa utawala wa kikoloni hakukuwa na nafasi ya kutosha kwa Watanganyika na Wazanzibari
kusimamia na kujieleza kwa uhuru kuhusu haki zao na harakati za ukombozi.
Ø Badala
yake, mambo mengi ya harakati za kudai uhuru yalifanyika kwa siri kuhofia
adhabu kutoka kwa wakoloni.
Ø Viongozi
na wanachama wa TANU na ASP waliamua kutumia sanaa na michezo kama mbinu
mbadala.
Ø Sanaa
ilitumika katika kukuza na kuendeleza harakati za kudai uhuru wa Tanganyika na
Zanzibar. Walianzisha vikundi na vyama vya sanaa na michezo kama vile kikundi
cha taarabu cha Jipisheni (Egyptian Music Club) na Al-Watan
Ø Vikundi
hivyo vilikuwa vinafanya matamasha na mwalimu Nyerere alialikwa kama mgeni
rasmi. Mwalimu nyerere alisimama kufungua hafla hizo na kwa kufanya hivyo,
alisema maneno machache kuhusu harakati za kudai uhuru
Ø Vilevile
kupitia taarabu, TANU ilikusanya fedha kwa ajili ya kuendeleza harakati za
ukombozi
H: VYAMA
VYA SIASA
v Umoja
wa Waafrika ulioitwa African Association (AA) uliundwa mwaka 1929 na mnamo
mwaka 1948 ulipewa jina jipya la Tanganyika African Association (TAA).
Ø
Mwaka
1954, chama hiki kilibadilishwa jina tena na kuwa chama rasmi cha siasa kwa
jina la TANU.
Ø
TANU
ilikuwa na malengo mbalimbali kama vile;-
i.
Kuwaunganisha
wananchi wa Tanganyika na kuwaongoza katika mapambano ya kupigania uhuru wa nchi
yao,
ii.
Kutoa
tafsiri mpya ya ukombozi pamoja
iii.
Kuweka
juhudi na fikra mpya za mapambano kwa msingi wa kifalsafa
iv.
kudai
haki ya kuwa na wawakilishi wa kidemokrasia katika vyombo vya kutunga sharia
Ø
Vyama vingine ni kama vile;-
i.
United Tanganyika Party (UTP)
kilichoanzishwa mwaka 1956. Chama hiki kiliungwa mkono na wazungu, waasia na
baadhi ya waafrika, hasa machifu.
ii. African
National Congress (ANC) kilichojitenga kutoka TANU mwaka 1958 na kuongozwa na
Zuberi Mtemvu.
iii. All
Muslim National Union of Tanganyika (AMNUT). Chama hiki kilidai uhuru lakini
walitaka mabadiliko ya katiba na uhuru viletwe polepole na si haraka kama TANU
ilivyotaka.
Ø Mpaka
wakati wa uhuru, Tanganyika ilikuwa na vyama hivi vine
v Kwa upande wa Zanzibar, vyama
vilivyojitokeza kudai uhuru ni pamoja na
i.
Zanzibar Nationalist Party (ZNP)
kilichoanzishwa kwaka 1955,
ii. Afro-shirazi
Party (ASP) Kilichoanzishwa mwaka 1959.
Ø Vyama
vyote hivi vilikuwa na lengo kuu la kudai uhuru wao.
Ø
Chama
cha ASP kilikuwa na malengo ya
i.
kupigania uhuru wa Zanzibar,
ii. kuunda
serikali ya kidemokrasia katika visiwa vya unguja na pemba,
iii. kuondoa
ubaguzi wa aina yoyote katika visiwa hivyo,
iv. kudumisha
uhuru wa Zanzibar na watu wake
v. kuwaandaa
wananchi wawe tayari kupigania uhuru wao.
Mchango wa
TANU na ASP katika harakati za kudai uhuru Tanzania.
i.
Vyama vya TANU na ASP viliunganisha
wananchi na kuwaongoza katika mapambano ya kudai uhuru.
ii. Vilihamasisha
wananchi kujiunga navyo na kushiriki katika harakati za kuudai uhuru wan chi
zao.
iii. Vyama
hivi viliandaa mikutano ya kisiasa na kuhamasisha wanachama pamoja na wanachi
kuhudhuria mikutano hiyo.
iv. Vilitoa
elimu na mafunzo ya kiuongozi na kisiasa kwa viongozi wa matawi na kitaifa.
v. Vyama
vya TANU na ASP vilianzisha vyombo vya habari ili kuendeleza harakati za kudai
uhuru.
MCHANGO WA HARAKATI
ZA KUPINGA UVAMIZI NA UKOLONI
Mchango
wa harakati za kupinga uvamizi wa kikoloni ulikuwa ni pamoja na kutunza
maadili na kujenga uzalendo
1.
KUTUNZA MAADILI
Ø Ujenzi
wa maadili ni mchakato wa kihistoria kwa kuwa unatokana na hisia ambazo watu au
jamii wamezikuza kwa miaka mingi kama sehemu ya harakati zao za kuleta
maendeleo na uhuru katika jamii au nchi yao.
Ø Maadili
ni muhimu kutunza kwa vile yanaleta fahari, umoja, ujasiri, na mienendo
inayokubalika katika jamii.
Ø Hivyo,
harakati za kupinga ukoloni nazo zilichangia katika utunzaji wa utambulisho wa
mtanzania, ambao ni pamoja na utu, mshikamano na lugha ya Kiswahili.
A.
Kudumisha
umoja
Harakati
za kudai uhuru zilichangia pia kudumisha umoja.
Ø
Kabla ya uhuru, jamii za kitanzania
zilikuwa zimegawanyika katika makabila mbalimbali. Kila kabila lilikuwa na utaratibu wake wa maisha ikiwemo
mila na desturi zake.
Ø
Viongozi
wa vyama vya TANU na ASP waliunganisha makabila na jamii mbalimbali.
Ø
Hali
hii ilisaidia kudumisha maadili ya umoja kwani waliamini kuwa Umoja ni nguvu,
Utengano ni udhaifu.
B. Kutunza
na kudumisha maadili ya Utu.
Ukoloni na mifumo yake iliathiri sana utu wa waafrika na
hivyo kuamsha ari ya kupata uhuru ili kutunza maadili ya utu yaliyokuwa
yamejengwa na jamii za asili za Tanganyika na Zanzibar.
Ø
Kwa
hiyo, harakati za kupinga ukoloni pia zilichangia katika utunzaji na udumishaji
wa maadili ya utu, kwani watanzania hawakuwa tayari kuona utu wao au maadili
yao yakipotea
C.
Kudumisha
mshikamano
Wakati
wa kupinga uvamizi wa kikoloni, viongozi waliunganisha watu katika jamii zao
ili kuwa na nguvu za kupambana na uvamizi wa kikoloni.
Ø Viongozi
kama vile Mtwa Mkwawa wa wahehe, Mangi Meli wa Old moshi, Mtemi Isike wa
Unyanyembe na viongozi wengine walihamasisha watu wao kushikamana ili
kukabiliana na uvamizi wa wakoloni wa kijerumani
Ø Aidha,
wakati wa harakati za kudai uhuru wa Tanganyika na Zanzibar, viongozi
walihimiza mshikamano wa watanzania wote ili kuwawezesha Tanganyika na Zanzibar
kupata uhuru
D.
Kukuza
na kudumisha Kiswahili
Harakati
za kupinga ukoloni na kupigania uhuru wa Tanganyika na Zanzibar zilitumia lugha
ya Kiswahili kwa namna mbalimbali.
Ø Mathalani,
Kiswahili kilitumika kusaidia kuleta umoja na mshikamano miongoni wa wanachama
wa TANU na ASP pamoja na wananchi wote.
Ø Lugha
ya Kiswahili iliwaunganisha wananchi wa jamii tofauti tofauti haijalishi
makabila yao. Nyimbo, taarabu zilizokuwa zinatumiwa katika mapambano dhidi ya
wakoloni zilikuwa katika lugha ya Kiswahili.
Ø Vyombo
vya habari kama magazeti mbalimbali yalitumia lugha ya Kiswahili katika
kuelimisha na kutoa habari kwa wananchi kuhusu harakati za kupigania uhuru.
Ø Sera
na itikadi za TANU na ASP zilielezwa kwa lugha rahisi ya Kiswahili, hivyo
kurahisisha ufikishaji wa ujumbe kwa wananchi.
Hivyo
kupitia harakati za kudai uhuru, Kiswahili kilijiimarisha na kuenea zaidi
nchini.
2.
KUJENGA UZALENDO
Harakati
za kupinga ukoloni vilihusisha upiganaji wa vita dhidi ya wakoloni.
Ø Katika
harakati hizi, watanzania walionesha uzalendo kwa jamii zao pale waliposimama
kidete kuupinga uvamizi na utawala wa kikoloni kwa sera zao za unyonyaji na
ukandamizaji.
Ø Baadhi
ya watanzania waliochangia katika ujenzi wa uzalendo kwa jamii zao ni pamoja na
Abushiri bin Salim al-Harthi wa Pangani, Mangi Meli wa Old Moshi, Mtemi Isike
wa unyanyembe, Mtwa Mkwawa wa Iringa, Mwene Machemba wa Wayao, Nkosi Songea,
Mbano wa Wangoni na Liti Kidanka wa Singida
Ø Hivyo,
harakati za wazalendo hawa kupinga uvamizi wa kikoloni, ulichangia katika
ujenzi wa maadili ya uzalendo kwani wananchi walijitoa kushiriki katika vita na
ulinzi wa jamii zao.
Ø Harakati
za kupinga ukoloni zilipanda mbegu ya uzalendo kwa jamii za kitanzania, kupenda
jamii zao na hata kujitoa maisha yao kupambana dhidi ya uvamizi wa kikoloni.
Hali hii ilichangia katika ujenzi wa kizalendo ndani ya jamii zao na baadaye
kwa nchi nzima za Tanzania
Ø Aidha,
viongozi vya vyama vya TANU na ASP pamoja na viongozi wengine katika ngazi
mbalimbali walikuwa wazalendo, kwani, walitoa mchango muhimu katika kuanzisha
na kuendeleza harakati za kudai uhuru. Uzalendo wao ulidhihirika kupitia
ushiriki wao katika kuanzisha na kusimamia vyama vya siasa.
ZOEZI
1. Je,
unafikiri ni kwa nini harakati za kudai uhuru wa Tanganyika na Zanzibar
zilifanikiwa kuwaunganisha wananchi?
2. Kwanini
vyama vya TANU na ASP vilipata uungwaji mkono mkubwa ukivilinganisha na vyama
vingine vya siasa wakati wa kupigania uhuru?
3. Eleza
kwanini uhuru wa Tanganyika na Zanzibar unapaswa kulindwa
4. Fafanua
maadili yaliyodumishwa wakati wa harakati za kudai uhuru wa Tanganyika na
Zanzibar
5.
Kwa
kutumia mifano, eleza maana ya uzalendo
6.
Jadili
mchango wa viongozi wa kisiasa wa sasa katika kutunza maadili na kujenga
uzalendo
7.
Eleza
mchango wa mwalimu Julius Kambarage Nyerere na sheikh Abeid Amani Karume katika
kupatikana kwa uhuru wa Tanganyika na Zanzibar
MADA YA KWANZA:UKOLONI KATIKA JAMII ZA KITANZANIA
MADA YA PILI:UKOLONI KATIKA JAMII ZA KITANZANIA
MADA YA TATU: MAPAMBANO YA AWALI DHIDI YA UVAMIZI WA KIKOLONI
MADA YA NNE: HARAKATI ZA KUDAI UHURU WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR
MADA YA TANO: UJENZI WA TAIFA BAADA YA UKOLONI
MADA YA SITA: MAPINDUZI MATUKUFU YA ZANZIBAR

No comments:
Post a Comment